LIFAHAMU TATIZO LA USUGU WA DAWA (Antimicrobial resistance)

USUGU WA DAWA (ANTIMICROBIAL RESISTANCE) ni nini?
Hii ni hali ya  dawa kushindwa kuua/kutibu vimelea vya magonjwa iliyokusudiwa kuua pindi dawa hiyo inapotumiwa kutibu ugonjwa husika.

USUGU WA DAWA UNASABABISHWA NA NINI?
Kushindwa kwa dawa kutibu ugonjwa/ kuua vimelea vya magonjwa utokana na matumizi  ya dawa yasiyo sahihi ambayo upelekea vijimelea vya magonjwa kujiwekea kinga ya kuuliwa na dawa.

YAFUATAYO NI MATUMIZI YA DAWA YASIYO SAHIHI
  • Kutomaliza dozi ya dawa uliyopewa kutibu ugonjwa husika (Hii inajumuhisha pia kuacha kutumia dawa mara tu unapohisi nafuu)
  • Kutumia dawa bila ya kufanya vipimo ili kujua unasumbuliwa na ugonjwa gani ili utumie dawa sahihi
  • Kutokufuata maelekezo ya jinsi ya kutumia dawa kama ulivyoelekezwa na mtaalamu wa afya
  • Kuchangiana dawa na mtu mwingine(Hii upelekea kupunguza dozi  kwa mtu aliyekuwa anatumia ile dawa pia na wewe utakuwa hujatumia dozi kamili
  • Kutumia dawa isiyosahihi kutibu ugonjwa husika, (Mfano Kutumia dawa ya kutibu ugonjwa unaosababishwa na  Bakteria wakati unaumwa ugonjwa unaosababishwa na Virusi)


MADHARA YA USUGU WA DAWA
  • Kuongeza gharama za matibabu
  • Kukaa hospitalini kwa muda mrefu
  • Uweza kusababisha kifo kutokana na kushindikana kwa Ugonjwa  kutibika
NINI UFANYE KUZUIA  USUGU WA DAWA?
  • Hakikisha unamaliza dozi  ya dawa uliyopewa
  • Husitumie dawa bila kufanya vipimo kujua unasumbuliwa na ugonjwa gani ili upate dawa/tiba sahihi
  • Tumia dawa kama ulivyoelekezwa na mtaalamu wa afya
  • Dawa uliyopewa itumie pekee yako, Husichangiane dawa na mwenzako

NB: DAWA INATIBU IWAPO ITATUMIKA KWA USAHIHI NA IPASAVYO






                    


Comments

Follow Us